Mtumiaji wa Siri za Chumbani haruhusiwi kuweka taarifa binafsi ndani ya confession yake ambazo zinaweza kumtambua yeye au mtu mwingine.
Taarifa binafsi zinahusisha namba ya simu, barua pepe (Email), taarifa za malipo kama LIPA namba au control number, majina ya akaunti za mitandao ya kijamii kama Instagram, Facebook, Telegram, Twitter (X) au taarifa nyingine yoyote inayoweza kuvunja mfumo wa anonymous wa jukwaa hili.
Sheria hii imewekwa kwa sababu msingi mkuu wa Siri za Chumbani ni kulinda utambulisho wa watumiaji. Mtumiaji anatakiwa kushiriki ujumbe wake bila kuweka taarifa ambazo zinaweza kusababisha yeye au mtu mwingine kufahamika.
Confession yenye taarifa binafsi inaweza kuzuiwa na mfumo wetu wa ukaguzi na haitachapishwa kwenye majukwaa yetu. Katika baadhi ya mazingira, mtumiaji anaweza kuzuiwa kutumia huduma ya kutuma confession kwa muda maalum.